Corona Lyrics – Corona by Rayvanny – Download mp3 audio
Corona, corona, corona
Wote tumuombe Mungu kwa hili janga
Ikibidi lipite
Tujihadhari na tujikinge
Ili lisitufike
Habari kote duniani zimesambaa
Ugonjwa unaua na hauna tiba
Na wengi wetu masikini hatujiwezi
Mwenyezi Mungu kawe tiba
Watoto wetu mashule, aah
Mama zetu sokoni, aah
Kwenye vyombo vya usafiri
Makazini tujilindee
Osha mikono
Epuka mikusanyiko sio ya lazima
Na uonapo dalili
Mapema wahi hosipitali
Corona, corona, corona
Corona, corona, corona
Corona, corona, corona
Corona, corona, corona
Tanzania hatuwezi tukajiweka pembeni
Bila kuchukua hatua
Hatua zimeshaanza kuchukuliwa
Waziri wa wizara ya afya ameshazungumza
Ameshatoa tahadhari mbali mbali
Ambazo tunatakiwa kuzichukua
Napenda nirudie ndugu zangu watanzania
Kwamba ni vizuri sana tukaendelea
Kuchukua tahadhari kwa nguvu zote
Ugonjwa huu unaua
Na unaua kwa haraka sana
Tuwaombe ndugu zetu watanzania
Tusipuuze ugonjwa huu
Tusipuuze hata kidogo
Ni lazima tuanze kuchukuwa hatua
Za kujikinga na tatizo hili
Corona Lyrics
ALSO, SING TO – Sinaga Swagger 4 Lyrics – Young Killer Msodoki – New Song