Home NEWS Uko Salama Lyrics – Barnaba – New Song 2020

Uko Salama Lyrics – Barnaba – New Song 2020

0
Uko Salama Lyrics

Uko Salama Lyrics – Barnaba – Download Mp3 Audio

Verse One

Noo no, Noo no…

Sitaki ulie sababu yangu
Wewe si ndo pepo yangu
Salama eeh, uko salama eeh

Sitaki ulie sababu yangu
Wewe si ndo pepo yangu
Salama eeh, uko salama eeh

Ya nini nijichoshe mwili
Wakati sijapenda
Si bora tu ntulize akili
Mahala nilikopenda

Hata tai huruka wawili
Sababu wamependana
Si bora tu nitulize akili
Ya nini kufosiana

Love is furaha
You are my furaha, nakupenda
Love is furaha
You are my furaha, nakuzimia

Yaongeze mahaba
Kisha nikupende mara saba
Salama, uko salama my love
Nishajifunza kuwa nakaba
Siri za ndani usijetangaza
Salama, uko salama beiby

Chorus

Sitaki ulie sababu yangu
Wewe si ndo pepo yangu
Uko salama, uko salama beiby

Sitaki ulie sababu yangu
Wewe si ndo pepo yangu
Uko salama, uko salama eeh

Verse Two

Chunga penzi usiliweke nyufa
Ukaziba ukuta, penzi likaanguka
Penzi tamu kuzidi asali nani anapinga
Kisha jaribu ndo utajua umbali wa unapotaka

Beiby niwashie taa
Niko kwenye giza na
We ndo mwanga
Ndo mwanga, ndo mwanga
Ndo mwanga, ndo mwanga eeeh

Huko nyuma nishasuffer
Nishajaribu mpaka vichaa
Washaniumiza, niumiza eeeh

Yaongeze mahaba
Kisha nikupende mara saba
Salama, uko salama my love
Nishajifunza kuwa nakaba
Siri za ndani usijetangaza
Salama, uko salama beiby

Chorus

Sitaki ulie sababu yangu
Wewe si ndo pepo yangu
Uko salama, uko salama beiby

Sitaki ulie sababu yangu
Wewe si ndo pepo yangu
Uko salama, uko salama eeh

Verse Three

Furaha yangu ni kukuona unatabasamu
Hata kama siku utanipochoka mikononi
Haijalishi kwa maana nakupenda
Hisia zangu haziko wazi
Na wala hazijifichi mbele zako machoi
Si unaona eeeh

Ukiniita natabasamu
Ukinigusa tu napata goosebumps
Hahaha, ningepewa jina nikuchagulie
Ningekuita waridi

Bali na kuwa nawe tunalala kitanda kimoja
Na jinsi sifaidi
Natamani kumkaidi bosi niachane na kazi
Nijipe likizo nisichoke kabisa
Niweze kustarehe na wewe
Hata pumzi itakaponizimia niwe
Basi uwe wa mwisho maisha

Nawaza lini Mungu atanichukua
Je kifo changu kitakuwa mwisho na wewe?
Naomba iwe hivyo maana sitaweza bila wewe
Iwe duniani, mbinguni ahera
Maana kwangu una dhamani zaidi ya hela
Leo, kesho na mtondogoo

I LOVE YOU!

Sababu yangu
Wewe si ndo pepo yangu
Salama salama salama

Uko Salama Lyrics Credit – Barnaba

ALSO, SING TO – Hawataki Lyrics – K2ga – New Song 2020

Leave a Reply